ads

adds

RONALDO ADHIHIRISHA KUMBE UMRI NI NAMBA TU ,AIONGOZA URENO IKIIPASUA LITHUAN

Mshambuliaji wa klabu ya Juventus na taifa la Ureno ameendelea kuonyesha ubabe wa hali ya juu.mchezaji huyo alitajw kushuka kiwango hivi karibuni kwa kuwa na umri mkubwa


hapo jana usiku Ronaldo mwenye miaka 34 aliwanyamazisha wapinzani wake kwa kufunga mabao 3 kwenye ushindi wa mabao 6-0. Mabao  ya Ronaldo yalifungwa dakika 2 kwa penati, 22 na 65 huku mengine yakifungwa na Pizi 52 , Goncalo 57 na Bernado Silva dakika ya 63 dhidi ya  Lithuan kwenye mchezo wa kufuzu fainali za EURO2020.

Ronaldo ametiimiza mabao 98 kuifungia Ureno kwenye michezo 163  aliyolitumikia taifa lake.

Ureno ni bingwa mtetezi wa kombe hilo na ameendelea kufanya vyema kwenye hatua ya makundi ya kufuzu michuano hiyo akicheza michezo 7 akishinda 4 sare 2 na kufungwa 1 na kujikusanyia pointi 14 nyuma ya Ukrain huku Cristiano Ronaldo akiwa nafasi ya tatu kwenye uungaji akiwa na mabao 10 nyuma ya Harry Kane na Eran Zahavi wakiwa na mabao 11 kila mmoja 

Post a Comment

0 Comments