Montenegro katika kufuzu michuano ya Euro 2020kwa kosa la ugomvi.Kocha wa timu ya Taifa ya Uingereza amefafanua kuwa wamelazimika kuchukua uamuzi huo baada ya kuzuka ugomvi baina ya Raheem Sterling na Joe Gomes katika uwanja wa mazoezi wa St. George’s Park.
Ikumbukwe Sterling wa Manchester City, alitunishiana kifua na beki wa Liverpool, Joe Gomez, wakati wa ushindi wa Liverpool 3-1 huko Anfield Jumapili. Chama cha Waandishi wa habari England, kimeripoti kuwa wawili hao walizusha tafrani tena siku ya Jumatatu wakati wa mazoezi ya timu ya England.
Kocha wa England, Southgate amesema wamechukua uamuzi wa kutomjumuisha Raheem kwenye mechi dhidi ya Montenegro Alhamisi, na uamuzi huo umefanywa kwa makubaliano ya kikosi kizima cha England.
0 Comments