ads

adds

MESSI ALIPA KISASI BAADA YA KUFUNGIWA

Mchezaji bora kwenye tuzo za FIFA mwaka  2019 Lionel Messi ameendelea kuonyesha ubora wake ndani ya uwanja kwa kufanya vyema akiwa na Barcelona na Argentina



Messi alifungiwa mwezi Julai mwaka huu baada ya kulilaumu shirikisho la soka Amerika Kusini kupokea rushwa toka kwa timu ya taifa Brazil ili timu hiy iweze kutwaa kombe la COPA America madai ambayo chama hicho kiliyakataa na kumuadhibu faini ya $50,000 pamoja na kutocheza michezo 4 ya timu ya Taifa .

Messi amerejea kikosi cha timu ya Argentina kwa kishindo baada ya kufunga bao pekee kwenye mchezo wa kirafiki kati ya Brazil na Argentina mchezo uliomalizika kwa Argentina kushinda bao1-0  na kutwaa kombe maalum kwa ajili ya mchezo huo.



Kikosi cha Argentina kiliongozwa na Andrada,Foyth,Pezella ,Otamendi , Tgriafico,Ocampos, De Paul,Paredes,Lo Celso, Martinez na Lionel Messi.

Kwa upande wa Brazil kikosi hicho kiliongozwa Allison,Danillo,Militao,Thiago Silva,Sandro,Arthur ,Casemiro,Lucas Paqueta,Gabriel Jesus ,Firmino na Willian.


Post a Comment

0 Comments