MAKAME NA MNATA KUONDOKA YANGA HIVI KARIBUNI ,CHANZO CHATAJWA

 Wachezaji wa Klabu ya Yanga Metacha mnata na Abdulaziz Makame wanaweza kuondoka klabuni hapo wakati wowote mbali na kwamba wana mikataba na klabu ya Yanga 


Makame na Metacha wamesajiliwa msimu huu na wamefanikiwa kuingia mkataba na kampuni ya  
 AfriSoccer ambayo inahusika na uwakala wa kuwatafutia wachezaji timu nje ya nchi

Baada ya kuona uwezo wa wachezaji hao Kampuni hiyo ilifikisha taarifa kwa wachezaji na uongozi wa Yanga na wamefanikiwa kuwasajili Metacha


Nyota hao ambao pia wako timu ya Taifa, watakuwa na nafasi ya kujaribu bahati yao nje ya nchi kama zitatokea timu kuwahitaji . Wachezaji hao bado wana mikataba na Yanga, ikitokea timu kuwahitaji, italazimika kumalizana na Yanga. 

Post a Comment

0 Comments