ads

adds

MAJERAHA YANAVYOZIDI KUMMALIZA NEYMAR JR

Mshambuliaji ghali zaidi Duniani anayechezea timu ya taifa Brazil na klabu tajiri ya Paris Saint German amekumbwa na balaa la kuumia mara kwa mara hivyo kushindwa kuonyesha ubora wake.



Kwenye mchezo wa kirafiki ulioigwa jana jumapili Neymar alitolewa nje ya uwanja dakika ya 12 tu toka mpira uanze akihofiwa kuata majeraha ya kifundo cha mguu.

Mchezaji huyo mwenye miaka 26 amekuwa akisumbuliwa na tatizo hilo hivyo kumpelekea kukaa benchi mechi mbalimbali za ligi kuu Ufaransa.

Mwaka huu Neymar alishindwa kuisaidia timu ya taifa Brazil iliyocheza Copa America na kutwa  kombe hilo nchini Brazil kutokana na majeraha.

Neymar alirejea mwezi Septemba 14 dhidi ya Strasbourg mchezo wa ligi kuu Ufaransa na alifunga bao la ushindi. Mechi nyingine alizoshiriki na kufunga ni pamoja na Bordeaux na Lyon.

Kuumia mara kwa mara kumemfanya nyota huyo ushindwa kuonyesha uwezo wake halisi

Post a Comment

0 Comments