ads

adds

DAVID LUIZ ATUA RWANDA KUWASHUHUDIA TAIFA STARS

Mchezaji wa Klabu ya Arsenal na timu ya taifa Brazil ametua nchini Rwanda na inaaminika ameenda  kuitazama Taifa Stars inayokipiga na Rwanda wikiendi hii


Rwanda inaidhamini timu ya Arsenal tangu msimu uliopita kupitia kampeni yake ya " VISIT RWANDA". Mchezaji huyo wa Arsenal alipokelewa na raisi wa nchi hiyo Mhe. Paul Kagame ofisini kwake.

Rwanda imekuw ikiitumia Arsenal Kujitangaza na Paul Kagame amefanikiwa sana kutumia mbnu hiyo kwani watalii wengi wamekuwa wakifika nhini humo. Jambo jinge ni kuruhusu makampuni kusajiliwa bila tozo zozote nchini Rwanda.

Luiz ataondoka nchini Rwanda mara baada ya mchezo wa Taifa Staz na Rwanda kumalizika na anatarajiwa kuwa mgeni rasmi wa mechi hiyo.

Mara baada ya picha za Luiz kusambazwa mkundi mbalimbali yameonekana kufurahi na kuahidi kufurika uwanjani hapo ili waweze kumwona nyota huyo.

Post a Comment

0 Comments