Yakiwa yamesalia masaa machache kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa Afrika kocha wa klabu ya Yanga Bw.Mwinyi Zahera ameonyesha kujiamini na kushinda mechi hiyo.
Kocha huyo wa Yanga ameizungumzia Zesco kama ni klabu kubwa na inacheza michezo mingi lakini anaamini atawafungwa kwani anafahamu mbinu wanazotumia na ameona hayo kupitia CD mbalimbali alizotumiwa na kocha wa TP Mazembe.
Mbali na Kumkosa Molinga na Mustafa kocha huyo amesisitiza kuwa wachezaji waliopo wamekamilika na watafanya vizuri.
Endapo Yanga itafanya vizuri hatua hii basi itaingia hatua ya Makundi ya ligi ya mabingwa Afrika.
0 Comments