ads

adds

BENZEMA AWEKA REKODI MPYA REAL MADRID

Karim Benzema ameingia katika orodha ya wafungaji  wa muda wote Real Madrid ila anakazi ya ziada kuvunja rekodi ya Ronaldo.
Goli dhidi ya Getafe alilofunga wikiendi iliyopita limemfanya ashike nafasi ya 7 katika orodha hiyo akiwa na magoli 182 sawa na Fransco Gento aliefanya hivyo msimu wa 1952-1970.
Benzema amefunga magoli 123 ya La Liga, 39 ligi ya mabingwa ulaya, 15 copa del Rey na 3 kombe la dunia ngazi ya vilabu.
Katika orodha iliyotolewa na na FIFA Ferenc Puskas (242), Carlos Santillana ( 290), Alfredo di Stefano (308), Raul Gonzalez (323) na Cristiano Ronaldo (412). na wote walikuwa na miaka 29.

Je Benzema ataweza kuwa mfungaji bora wa muda wote akimzidi Ronaldo?

Post a Comment

0 Comments