ads

adds

CARVAJAL KUKIPIGA MADRID MPAKA 2022

Klabu ya Real Madrid imemwongeza beki wake Daniel Carvajal mkataba utakaodumu mpaka 2022.
Carvajal alijiunga na miamba hiyo ya hispania akitokea Bayern leverkusen m2013 na kuisaidia timu hiyo kubeba ligi ya mabingwa ulaya mara 3 na ligi kuu hispania mara moja.

Klabu hiyo imefikia uamuzi wa kumwongeza mkataba kutokana na beki huyo kuwa nguzo ya ukabaji upande wa kulia , klabu hiyo imemuongeza mkataba mwingine mpaka 2022 wakati ule wa awali ungekwisha mwaka
2020 .

Carvajal anaungana na wachezaji wengine kama isco na Marcelo waliopewa mikataba mipya na timu hiyo

Post a Comment

0 Comments