Sahau kuhusu Mohammed Salah pale Ivory Coast kuna huyu bwana mkubwa wa kuitwa Mustafa Mohammed anayekipiga Nantes pale Ligue 1 Ufaransa. Huyu ndiye mchezaji hatari zaidi katika kikosi cha Egypt kwenye michuano inayoendelea .
Mpaka sasa nyota huyu amefunga mabao 3 katika michezo mitatu aliyocheza hatua ya makundi na mabao yake yameisaidia Misri kutinga hatua ya robo fainali kibabe.
Nyota huyu anawania Kiatu cha Ufungaji Bora akiwa na mabao 3 huku mfungaji anayeongoza mbio hizo ni Emilio Nsue Lopez wa Equatorial Guinea.
Mchezo wa kwanza kati ya Misri dhidi ya Cape Verde ulimalizika kwa timu hizo kutoka sare ya mabao 2-2 nyota huyu alitupia bAo dakika ya 4 ya mchezo huo.
Mchezo wa pili dhidi ya Ghana uliomalizika kwa sare ya mabao 2-2 nyota huyu alitupia bao moja la Misri
Mchezo wa mwisho dhidi ya Mozambique uliomalizika kwa sare ya mabao 2-2 nyota huyu alifanikiwa kufunga dakika ya 90+3 na kuisaidia timu yake kuingia hatua ya robo fainali .
Katika kundi B ni Cape Verde pekee amefanikiwa kushinda mechi 2 na sare 1 wakijikusanyia point 7 ,Misri wao wamemaliza nafasi ya pili wakiwa na pointi 3 na michezo yote wamesuluhu.Ghana wamemaliza michuano hiyo wakiwa na pointi 2 baada ya kusare Michezo 2 na kufungwa mmoja .Mozambique wao wamepata sare 2 na kufungwa mchezo mmoja.
Haya hapa matokeo ya Misri hatua ya makundi
0 Comments