ads

adds

MO DEWJI AMWAGA MABILIONI KWENYE MASUMBWI KINA MWAKINYO ,MANDONGA KAZI KWENU

Hatimaye Mwekezaji na Mmiliki wa makampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited bwana Mohammed Dewji ametangaza ujio wa pambano la Masumbwi lililochini ya kampuni yake ya MOBOXING. Mwanzoni mwa mwezi June Dewji alitangaza ujio wa kampuni hiyo na sasa anza kazi imekwishaanza kwa pambano la kimataifa litakalowakutanisha mtanzania Ibrahim Classic na mmexico Alan Pina.


Pambano hilo litapigwa Septemba 30 katika Hotel ya Next Door Arena na linategemewa kuwa na watazamaji wengi huku pia makampuni ya kurusha tangazo hilo mbashara yakikaribishwa kudhamini pambano hilo kubwa na la kwanza kwa kampuni ya MOBOXING

Taarifa kutoka kwa watu wa karibu na Mohammed Dewji zinasema tajiri huyo amedhamilia kuwekeza pesa nyingi kwa mchezo wa masumbwi na kubadilisha maisha ya vijana wanaoutumikia mchezo huo. Kuwekeza ndani ya boxing kutawafanya watanzania wengi wanufaike na kupunguza tatizo la ajira nchini.Mohammed Dewji ambaye pia mmiliki wa hisa 49% ndani ya Simba amekuwa msaada mkubwa kwa vijana akiwapa ajira kupitia viwanda vyake na fursa ya kusomeshwa kwa wanafunzi wasiojiweza kiuchumi kupitia taasisi ya MO DEWJI FOUNDATION. 

Uongozi wa AMOSPOTI HOLDINGS TANZANIA LTD kupitia mkurugenzi wake Bw.Amos Medeck  upo tayari kuungana na MoBoxing kulitangaza pambano hili mubashara kupitia mitandao ya kijamii

0694021861

Post a Comment

0 Comments