advertise with us

ADVERTISE HERE

CV YA KOCHA MPYA WA AZAM YAWAFUNIKA ZOLAN MAKI, PROFESA NABI

Hatmaye klabu ya Azam imefanikiwa kumpata kocha Denis Lavagne raia wa Ufaransa mwenye rekodi nzuri kwa soka la Africa.Kocha huyo anakuja kuchukua nafasi ya iliyoachwa wazi baada ya aliyekuwa kocha mkuu Bw. Moalini kupelekwa kusimamia timu ya vijana.


Azam wamefanya mabadiliko makubwa ndani ya kikosi chao kwa kuwasajili wachezaji wa kimataifa na wenye umri mdogo huku pia wakiimalisha benchi la ufundi kwa kuwaleta madaktari,makocha wa viungo,washambuliaji ,makipa na sasa wamemuongeza Denis Lavagne kama kocha mkuu.

Kocha Denis Lavagne amekwishawahi kuwa mchezaji wa timu mbalimbali za ufaransa tangu mwaka 1981  akicheza nafasi ya ulinzi na baada ya kustaafu alijiunga na kozi za ukocha mwaka 1989. Hizi ni timu ambazo Denis Lavagne amekwishazichezea mpaka sasa.


Apps
(Gls)
1981–1982Le Havre B
1982–1983Rouen B
1983–1984Béziers
1984–1985Alès
1985–1987Orange
1987–1989Alès B

Kocha huyu mkuu anauzoefu na soka la Africa na pia anamiliki leseni kubwa ya UEFA Pro Licence.Rekodi zake zinaonyesha ameanza kufundisha soka mwaka 1998 na amefundisha jumla ya vilabu 14 na Azam itakuwa ni timu ya 15. mwaka 1998-99 alifundisha Deveze na Baadaye alijifundisha timu zifuatazo 

1999–2003Sedan B
2007–2008Coton Sport
2009–2011Coton Sport
2011–2012Cameroon
2013Étoile du Sahel
2013–2014Al Ittihad Alexandria
2014Najran
2014–2015Smouha
2015–2016MAS Fez
2016Free State Stars
2016–2017Al-Hilal
2018–2019CS Constantine
2021JS Kabylie
2021USM Alger
kwa CV hii kocha Denis anakuwa ndiye kocha mwenye leseni kubwa zaidi nchini akiwaunika makocha wa Simba ambaye ni Zoran Maki na kocha wa Yanga ambaye ni Nabi Nasredene .kocha huyo kwa sasa yupo safarini na kuna uwezekano akauwahi mchezo dhidi ya Yanga utakaopigwa leo majira ya saa 1:00 Usiku. 

Post a Comment

0 Comments