advertise with us

ADVERTISE HERE

MAPYA YAIBUKA KATI YA SIMBA NA MATOLA

Kaimu kocha mkuu wa Simba Selemani Matola anaweza kuendelea kusalia klabuni hapo kwa msimu ujao baada ya kufanya vizuri kwenye michezo miwili ya ligi kuu aliyocheza kama kocha mkuu wa timu na kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mbeya City na 3-1 dhidi ya KMC. 


Matola anaamini anatosha kuwa kocha mkuu wa Simba lakini suala hiyo kwa sasa anawaachia mabosi wake ikizingatiwa kwamba nyota huyo wa zamani wa Simba ameitumikia Simba kwa miaka 5 mfululizo kama kocha msaidizi  na baadaye kama kaimu kocha mkuu baada ya aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo Franco Martinez kuondoshwa klabuni hapo kwa mwenendo mbaya.

Mara baada ya mchezo dhidi ya KMC kumalizika Matola alinukuliwa akisema 
"Nashukuru kwa nafasi hii niliyopo sasa ,tunaenda kujipanga kwa ajili ya mechi zilizobaki ili uhakikisha tunashinda zote na kumaliza vizuri,

"Kuhusu msimu ujao kuna mambo bado hayajakamilika ,yapo kwenye uongozi na yakikamilika basi mtajulishwa nini kinafuata ila sasa muda bado na nasikilizia kila kitu kikikaa sawa"

Post a Comment

0 Comments