BETI NASI UTAJIRIKE

NAMUNGO YATUMA SALAMU SIMBA,YANGA NA AZAMU FC MAPINDUZI CUP

 Klabu ya Namungo imetuma salamu kwa timu shiriki za michuano ya Mapinduzi Cup inayochezwa Zanzibar baada ya kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Meli 4 City mchezo uliopigwa uwanja wa Amani.


Mabao ya Namungo yalifungwa na Ali Saleh aliyefunga bao la kwanza dakika ya 21 huku bao la pili likifungwa na Obrey Chirwa dakika ya 80 kwa mkwaju wa penati huku Hussein Mwinyi akifunga bao la kufuta machozi dakika ya 90. Matokeo hayo yanaifanya Namungo kuongoza kundi A.


Post a Comment

0 Comments