Aliyekuwa mtangazaji wa Azam TV Ahmed Ally katika vipindi mbali mbali kikiwemo cha mshikemshike viwanjani ,Vitasa pamoja na kuhoji wachambuzi katika mechi mbalimbali
ametangazwa Rasmi kama Afisa habari wa klabu ya Simba akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Haji Manara aliyehamia Yanga tangu kuanza kwa msimu wa 2021/22. Ahmed Ally ameacha rasmi nafasi zote za utangazaji ndni ya Azam TV na sasa anakwenda kuanza majukumu mapya ndani ya Simba huku akitoa neno la shukrani kwa mashabiki zake wote na ameandika 'akikaa nitawamic kwelikwelii!!!! '
Ahmed Ally amepokea pongezi nyingi hasa kwa mashabiki wa Simba wakimkaribisha kwa bashasha wafanyakazi wa wenzake wa AZam TV wakimtakia heri na mafanikio katikam teuzi hiyo
Baraka Mpenja ameandika Ndugu OFISA HABARI NA MAWASILIANO JIPYA LA @simbasctanzania , AHMED ALLY AHMED @ahmedally_ , Tangazaji mahiri kutoka @azamtvtz.Hongera sana 👍👍👍💪Mwanangu🔥🔥🔥
Ally Kamwe ameandika 🚨Ukipenda unaweza kumuita AHMED SIMBA 🦁 Hilo ALLY tulitoeni kwa muda 😃
Hashim Ibwe ameandika KAZI TUNAYO NA NI KAZI KWELI KWELI 😂😂😂😂😂😂😂😂.Kila la kheri Kaka 🙏🙏🙏🙏🙏
Afisa habari na mawasiliano Simba sc
0 Comments