NEW CASTLE WAANZA TIMUA TIMUA,MOURINHO ATAJWA

 Baada ya kufanikisha kuuza hisa 8% kwa dau la dola milioni 300 uongozi wa Newcastle umeanza kutimua baadhi ya watu muhimu akiwamo kocha mkuu wa klabu hiyo Steve Bruce. Taarifa rasmi imesema imeamua kuachana na kocha huyo aliyejiunga na klabu hiyo msimu wa 2019/20

Nafasi ya Bruce imechukuliwa na Graeme James na kazi hiyo amekwisha anza kuelekea mchezo dhidi ya Crystal Palace. kupitia barua hiyo imesema "New Castle inathibitisha kuachana na aliyekuwa kocha Mkuu Steve Bruce kwa makubaliano ya pande zote mbili ,na Graeme Jones atakaimu nafasi hiyo kuanzia sasa kuelekea mchezo dhidi ya Crystal Palace"

Taarifa za ndani zinasema Kocha wa AS ROMA Jose Mourinho anatajwa kuja kuanza kazi mwanzoni mwa kwaka 2022 na hata alipoulizwa kuhusu nafasi hiyo alikiri kwa kusema anamahusiano mazuri na uongozi wa klabu hiyo ingawa kwa sasa yupo AS ROMA

Post a Comment

0 Comments