YANGA WATOA TAARIFA MAENDELEO YA BALAMA MAPINDUZI

Uongozi wa Yanga kupitia Afisa Habari  wake Hassan Bumbuli umetoa taarifa kuhusiana na Kiungo wa Yanga Balama Mapinduzi ambaye yupo nchini Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu. Taarifa hiyo imesema Balama amekamilisha awamu ya kwanza ya matibabu baada ya kukamilisha vipimo nchini humo.
Balama ataingia awamu ya pili ya matibabu yake kuanzia leo na Hassan Bumbuli amesema awamu ya kwanza ilikuwa ni vipimo vya aina tatu , ambavyo vimekamilika

Kinachofuata ni Madaktari kuona matibabu gani yanafaa baada ya kujiridhisha na majibu ya vipimo
Bumbuli amesema madaktari wamegundua kwamba mfupa uliunga vibaya hali ambayo ilikuwa ikimsababisha maumivu aliyokuwa akiyapata wakati alipoanza mazoezi mepesi

Post a Comment

0 Comments