FIFA YATOA KIKOSI BORA CHA MWAKA 2020 LIVERPOOL YAFUNIKA

 Shirika la mpira Duniani FiFA limetoa orodha ya wachezaji 11 wanaounda kikosi bora cha dunia kwa mwaka 2020. Kikosi hicho kimetoa wachezaji kutoka timu mbali mbali huku Bayern Munich ikitoa wachezaji 3 Liverpool wachezaji 4 ,ReAL madrid 1,Barcelona 1 ,Mancity 1 na Juventus 1

Klabu ya Liverpool imetoa wachezaji wanne akiwemo kipa Alisson beki Anord na Van Dijk pamoja na kiungo Thiago Alcantara aliyehamia klabunio hapo mwezi Septemba akitokea Bayern Munich alikoisaidia timu hiyo kutwaa makombe ya Uefa,Bundesliga na kombe la ligi.

Bayern Munich imemtoa beki kinda Alphonse Davies ,kiungo Joshua Kimich pamoja na mshambuliaji Robert Lewandowski. Real Madrid wao wamemtoa Sergio Ramos ,Barcelona wakimtoa Messi na Juventus wakimtoa Ronaldo Cristiano.


Post a Comment

0 Comments