ads

adds

SIMBA WAFAFANUA SUALA LA USAJILI WA MORRISON


Uongozi wa Simba kupitia afisa habari wake Haji Manara umesema kuwa mchezaji mpya wa timu hiyo Benard Morrison alikwisha malizana na Yanga na hakuna kesi yoyote inayomkabili.  Manara amenukuliwa akisema 

"Kesi ya kimkataba ina uhisiano gani na Morrison kusajiliwa, mchezaji kafika tarehhe 17 wao wanasema wamemsajili tarehe 15 inaoneshwa kwamba mkataba wa kwanza umesajiliwa tarehe 15, Yanga wamemuingiza kwenye mkataba tarehe 15 sasa kwahiyo hapo wajadili suala la mkataba wa kwanza.

"Waache kutuchezea mambo ya ajabu, tarehe 15 dirisha dogo la usajili lilifungwa, Morrison alitua nchini tarehe 17 sasa hapo anzeni pale, kuna mkataba ambao umesainiwa kwenye page nne sasa mkataba wa Morriosn una page moja kwa nini?

"Kamati ya hadhi ya wachezaji haiwezi kufanya mambo ya ajabuajabu, cha kwanza kiangaliwe mkataba wa kwanza kama ni halali ama sio halali, hivyo amecheza mechi za Singida na Tanzania Prisons akiwa hana mkataba, mkataba wake unaonyesha kwamba amesajiliwa kabla ya muda," amesema.

Post a Comment

0 Comments