advertise with us

ADVERTISE HERE

TETESI ZA SOKA DUNIAN LEO ALHAMISI TAREHE 18-06-2020

Manchester United imefanya mawasiliano na wawakilishi wa Willian kuzungumzia uhamisho huru kwa ajili ya mshambuliaji huyo, 31, ambaye mkataba wake na Chelsea umefika ukingoni msimu huu. (France Football-in French)


Kocha wa Everton Carlo Ancelotti ameanza mazungumzo na klabu ya zamani ya Napoli kuhusu kiungo wa Kireno Allan, 29. (Express)

Ancelotti pia anajaribu kumsajili Mbrazili anayekipiga St-Germain katika nafasi ya ulinzi Thiago Silva kwa uhamisho huru, mara tu mkataba wake utakapokwisha msimu huu. (Express).

Gareth Bale celebrates with Wales after reaching the semi-final of Euro 2016Haki miliki ya picha

Mahusiano ya Gareth Bale na kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane yamefikia hatua ya kushindikana, lakini mshambuliajii huyu ameendelea kuwa na furaha. (Marca)

Mustakabali wa Jadon Sancho kwenye kikosi cha Borussia Dortmund bado umekuwa si wa uhakika baada ya kocha mkuu Lucien Favre kumuorodhesha mshambuliaji huyo,20, kuwa miongoni mwa wachezaji ambao wanaweza kuondoka msimu huu. (Sky Sports)

Kocha wa RB Leipzig Julian Nagelsmann amesisitiza kuwa Timo Werner, 24, bado yuko kwenye mipango ya timu hiyo kwa ajili ya ligi ya Champions, ingawa mshambuliaji huyo amekubaliana na Chelsea. (Mirror)

Moussa DembeleHaki miliki ya picha

Leicester City imejiunga kwenye kinyang'anyiro na Manchester United kumnasa mshambuliaji wa Lyon, Moussa Dembele. (France Football, via Leicesteshire Live)

Chelsea imeongezewa nguvu katika mbio zake za kumnasa Kai Havertz huku Bayern Leverkunsen ikisema hawata 'mzuia' iwapo atataka kuondoka baada ya kiungo huyo Mjerumani, 21 kusema anahitaji changamoto mpya. (Kolner Stadt-Anzeiger-in German)

Post a Comment

0 Comments