advertise with us

ADVERTISE HERE

REAL MADRID YAENDELEZA UBABE LA LIGA ,BENZEMA AZIDI KUMKARIBIA MESSI


Kikosi cha Real Madrid kimeonyesha uwezo wa hali ya juu kwenye mchezo wa ligi kuu nchini Hispania baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Valencia . Mchezo huu ni wa 29 kwa Real Madrid wenye pointi 62 wakiwa nyuma ya Barcelona wenye pointi 64.

Karim Benzema alikuwa kwenye ubora wake baada ya kufunga mabao  dakika ya 61 na 86  huku Asensio akifunga bao moja dakika ya 74.Madrid walikuwa imara  kuandia eneo la ulinzi kwa kuruhusu mashuti mawili tu kulenga golini kati ya 6 yaliyopigwa na Valencia.

Eneo la kiungo lilimilikiwa vyema na Casemiro ,Modric na Kroos na kuwafanya kuutawala mchezo kwa asilimia 59 dhidi ya 41 za Valencia . Eneo la ushambuliaji likiongozwa na Benzema ,Valverde/Asensio na Hazard/Vinicius lilikuwa imara baada ya kupiga mashuti 19 huku 16 yakilenga golini kwa Valencia.

Kikosi cha Real Madrid kiliongozwa na Coritous,Carvajal,Ramos,Varane ,F.Mendy,Kroos,Modric,Casemiro,Hazard/Vinicius,Valverde/Asenso na Benzema 

Valencia:Cillesen,Wass,Mangala,Guillamon,Gaya,Pajero,Torres,Kondobia,soler,Rodrigo na Gomez






Post a Comment

0 Comments