advertise with us

ADVERTISE HERE

MARTIAL AANDIKA HISTORIA MPYA NDANI YA MANCHESTER UNITED


Mshambuliaji wa Manchester United raia wa Ufaransa Antonio Martial ameweka historia mpya ndani ya manchester United baada ya kufunga mabao 3 (Hat Trick ) ndani ya Klabu hiyo.Mshambuliaji huyo mwenye miaka 24 alikuwa mwiba mkali kwa Shiffield United baada ya kufunga mabao dakika ya 7,44 na 74. na kuifanya Manchester United kuibuka na ushindi wa mabao 3-0

Martial anakuwa mchezaji wa kwanza wa Manchester United kufunga Hat trick ndani ya Premier League tangu kuondoka kwa Alex Ferguson mwaka 2013. Mchezaji wa mwisho kufunga Hat trick kabla ya Martial ni Robin Van Persie mwaka 2013 dhidi ya Aston Villa.

Msimu wa 2019/20 umekuwa bora zaidi kwa Martial baada ya kufunga mabao 14 kwenye michezo 25 aliyocheza tangu kusajiliwa kwake mwaka 2015 akitokea Monaco ya Ufaransa.


Post a Comment

0 Comments