advertise with us

ADVERTISE HERE

LA LIGA: BARCELONA VS ATLETICO MADRID UPO WAPI LEO


Ligi kuu nchini Uhipania inaendelea leo usiku kwa kuikutanisha miamba mbalimbali inayoshiriki La Liga .Mallorca atakuwa nyumbani dhidi ya Celta vigo,Leganes vs Sevilla huku Barcelona akimkaribisha Atletico Madrid dimba la Nou Camp.

Barcelona anatakiwa kushinda mchezo huo ili kurejea kileleni baada ya Real Madrid kushinda mechi dhidi ya Espanyol na kuwafaya waongoze ligi kwa pointi 71 dhidi ya 69 za Barcelona.

Endapo Barcelona atafungwa mchezo huo basi atakuwa na kibarua kigumu kutwaa La Liga  kwa msimu huu kutokana na uchache wa mechi zilizobaki. Atletico Madrid na yeye anakazi ya ziada kwa kushinda mchezo dhidi ya Barcelona ali aendelee kubaki nafasi ya 3.

Lionel Messi atakuwa na kazi moja tu ya kufunga bao lake la 700 tangu alipoanza kucheza soka la kulipwa.

Post a Comment

0 Comments