ads

adds

HIVI NDIVYO LIGI KUU UINGEREZA ITAKAVYOPIGWA KWA STAILI MPYA WIKI IJAYO

Wachezaji na makocha wa Ligi ya Primia ya England hawatalazika kuvaa barakoa uwanjani mara ligi hiyo itakaporejea wiki ijayo.
Hata hivyo wachezaji hawatatakiwa kutema mate uwanjani au kusafisha pua zao na kutokumbatiana wakati wa kushangilia magoli.
Pia hakutakuwa na watoto wa kuwarushia wachezaji mipira inayotoka nje, na badala yake mfumo maalumu wa mipira iliyosafishwa utatumika.
Aston Villa v Sheffield United utakuwa mchezo wa kwanza wa EPL utakaofungua tena pazia la EPL Juni 17.
Ligi hiyo ilisimamishwa mwezi Machi kutokana na mlipuko wa virusi vya corona.
Nchini Ujerumani wachezaji, makocha na Magila wengine wa ligi ya Bundesliga wanatakiwa kuvaa barakoa muda wote isipokuwa muda wa mechi.
Katika ligi ya EPL hawatatakiwa kuvaa barakoa kabisa, hata katika vyumba vya kubadili na kwenye mabenchi ya makocha na wachezaji wa akiba.



Hata hivyo, kamisaa wa mchezo na madaktari wa timu watatakiwa kuvaa barakoa.
Jana Alhamisi uongozi wa EPL ulitangaza kuwa kutakuwa na ukimya wa dakika moja katika mechi zote za awali kwa lengo ili kuwakumbuka wale wote waliopoteza maisha katika janga hili.
Beji maalumu za umbo la kopa zitavaliwa na wachezaji kwa lengo la kuwashukuru wahudumu wa afya na wafanyazi wengine waliokuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya corona.
Klabu za EPL zimekubaliana pia kuhusu kanuni kadhaa za kiafya ambazo zitatekelezwa kwenye mechi zote zijazo.
Idadi ya watakaoruhusiwa uwanjani itadhibitiwa na viwanja vitagawiwa katika maeneo maalumu ili kuzuia mchangamano usio wa lazima.
Kwa ujumla, watu wataotakiwa kuwepo uwanjani hawatazidi 300 na katika 'eneo jekundu' hawatatakiwa kuzidi 110 ikiwemo wachezaji na maafisa wa klabu.

A staff member disinfects footballs at AnfieldHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES

Kutafanyika usafi wa hali ya juu wa maeneo ya vibendera vya kona, milingoti ya magoli, vibao vya kubali wachezaji na mipira kabla na baada ya kila mechi.
Kanuni hizo pia zinaeleza namna gani wachezaji na makocha watakavyosafiri kwenda kwenye mechi na kurudi.
Klabu zitashauriwa kusafiri kwa ndege kwenye mechi za mbali na kupunguza matumizi ya hoteli.
Wachezaji wote na makocha watapimwa joto la mwili kabla ya kuwasili kiwanjani.
Wachezaji pia watatakiwa kutumia vitakasa mikono kabla ya kuingia kiwanjani na wakitoka.

Post a Comment

0 Comments