ads

adds

BAADA YA SARE NA RUVU SHOOTING SIMBA YALIPIZA KISASI KWA TRANSIT CAMP

Klabu ya Simba imeonekana kukerwa na sare waliyoipata kwenye mchezo wa ligi kuu Tanzania bara dhidi ya Ruvu shootting mchezo uliopigwa jana dimba la taifa jijini Dar es salaam . 

Simba walilazimshwa sare ya mabao 1-1 na matokeo hayo yamewafanya kuendelea kuongoza ligi kuu baada ya kufikisha alama 72 

Leo asubuhi kikosi hicho kimecheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Transit Camp dimba la uhuru jijini Dar es salaam na mchezo huo umemalizika kwa Simba kushinda mabao 4-0.

Ibrahim Ajibu alikuwa wa kwanza kuzifumania nyavu za transit camp dakika ya 16 huku Gerson Fraga akifunga mabao mawili dakika ya 31 na 45 na Cyprian Kipenye akifunga bao la nne dakika ya 86.

Simba inajiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mwadui mchezo utakaopigwa siku ya jumamosi tarehe 20 wiki hii

Picha za mechi kati ya Simba vs Transit Camp






Post a Comment

0 Comments