CHUMA CHA LIPULI FC CHATAJWA KUREJEA YANGA


Nahodha wa Lipuli Paul Nonga ametupia mabao 11 na pasi nne za mabao na Lipuli ipo nafasi ya 13 baada ya kucheza mechi  29 na ina pointi 33 ikiwa imetupia mabao 35.
Nonga anatajwa kuwa kwenye rada za mabosi wa Kariakoo Yanga ambao wanahitaji kupata saini yake ya nyita huyo aliyewahi kuichezea timu hiyo na kuomba kusepa baada ya kukosa namba kikosi cha kwanza.
Kwa sasa amekuwa kwenye ubora wake na inaelezwa kuwa amewaambia mabosi wake Lipuli kwamba anahitaji kusepa ndani ya klabu hiyo ili apate changamoto mpya.

Nonga amewahi kuitumikia Yanga chini ya kocha Pluijim msimu wa 2015/16 na aisajiliwa dirisha dogo lakini hakufanya vyema kutokana na kukosa nafasi hivyo aliondoshwa ndani ya kikosi hicho cha Jangwani  baada ya miezi 6 tu kuitumikia timu hiyo.

Post a Comment

0 Comments