BETI NASI UTAJIRIKE

HAJI MANARA ALAMBA MAMILIONI YA LA LIGA ,ATAKA WAPINZANI WASITUMIE MAJINI



Msemaji wa klabu ya Simba ameendelea kula shavu baada ya kupata ubalozi wa La Liga nchini Tanzania. Hivi karibuni Manara alisafiri mpaka nchini ujerumani kusaini mkataba na chama cha soka Hispania kinachosimamia ligi ya La Liga 

Akiwa Uhispania manara atatembelea vilabu mbalimbali vinavyoshiriki La Liga na hapo jana alitembelea klabu ya Real Betis na walimkabithi jezi yenye jina lake la utani "DE LE BOSS"

Kwa upande mwingine Manara alitumia press ofisi ya Real Betis  kupiga promo mechi na watani zao wa jadi Yanga huku akitoa kauli kali zilizowakera mashabiki wa klabu ya Yanga .
Manara aliandika 


"Wakati Msemaji napata ruhusa ya kutumia press room ya @realbetisbalompie hapa Seville na kupiga promo juu ya game ya jumapili ,yupo Msemaji anahangaika na waganga na Majini huko Tanga.Kupanga ni kuchagua"



Post a Comment

0 Comments