Manchester United imeanza mazungumzo na beki wa kati wa Uholanzi Matthijs de Ligt, 24, ambaye yuko tayari kuondoka Bayern Munich msimu huu wa joto. (Sky Sport Germany)
Paris St-Germain wako tayari kulipa ada ya uhamisho iliyovunja rekodi ya dunia kumsajili winga wa Uhispania Lamine Yamal, 16, kutoka Barcelona. (Mundo Deportivo - in Spanish)
Manchester City wana nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Bayern Munich na Ujerumani Joshua Kimmich, 29, na winga wa RB Leipzig kutoka Uhispania Dani Olmo, 26. (Sun)
0 Comments