BETI NASI UTAJIRIKE

TETESI ZA SOKA DUNIANI LEO TAREHE 04 JULAI 2024

Manchester United ilifikiria kupata kitita kikubwa kutokana na mauzo ya nahodha Bruno Fernandes, 29, lakini kiungo huyo wa kati wa Ureno anatarajiwa kusalia katika klabu hiyo na kusaini mkataba mpya. (Mirror)



Ofa ya Arsenal ya euro milioni 47 ya kumnunua Riccardo Calafiori imekataliwa na klabu ya Bologna ambayo inataka angalau euro milioni 50 kumuuza mchezaji huyo wa kimataifa wa Italia. Chelsea pia wanavutiwa na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22. (Corriere dello Sport - kwa Kiitaliano)

Mchezaji huru Dele Alli ameonekana akifanya mazoezi kwa bidii huku akitafuta klabu mpya baada ya kuondoka Everton mkataba wake ulipokamilika mwishoni mwa msimu uliopita. (Express)

Beki wa Ufaransa William Saliba anaweza kuondoka Arsenal msimu huu huku Real Madrid wakimtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23. (Mirror)

Mshambuliaji wa Napoli Victor Osimhen, 25, anatarajiwa kuwa sehemu ya maandalizi ya klabu yake kwa msimu ujao wiki ijayo huku Manchester United, Chelsea na Arsenal zikiwa na nia ya kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Nigeria. (Football Italia)

West Ham wanafikiria kuwasilisha ofa mpya kwa mlinzi wa Nice Jean-Clair Todibo baada ya ofa ya pauni milioni 24.5 kwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa kukataliwa. (Mail)

Barcelona wanajaribu kumsajili mshambuliaji wa Uhispania Dani Olmo kutoka RB Leipzig, huku klabu hiyo ya Uhispania ikijitahidi kufikia na mpango wa malipo ili kutimiza kifungu cha kuachiwa cha euro 60m (£51m) cha mchezaji huyo wa miaka 26. (90 min)

Winga wa Brazil Willian amekataa ofa ya kandarasi mpya katika klabu ya Fulham, huku klabu za Saudi Arabia na Uturuki zikimtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 35. (Mail)

Kiungo wa kati wa Paris St-Germain Ethan Mbappe, kaka wa nahodha wa Ufaransa Kylian, anatarajiwa kusaini mkataba wa muda mrefu na Lille, kinda huyo mwenye umri wa miaka 17 hakuwahi kufanya mazungumzo na klabu mpya ya kaka yake Real Madrid. (Fabrizio Romano)

Everton wanavutiwa na mchezaji wa kimataifa wa Cameroon mwenye umri wa miaka 22 Jackson Tchatchoua huku klabu ya Hellas Verona ikitaka takribani euro milioni nane (£6.8m) kumuuza mlinzi huyo. (TuttoMercatoWeb - kwa Kiitaliano)

Atalanta wanatazamiwa kumsajili kiungo wa kati wa Italia Nicolo Zaniolo kwa mkopo kutoka klabu ya Uturuki ya Galatasaray ikiwa na jukumu la kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye alikuwa akiichezea klabu ya Aston Villa msimu uliopita, kwa mkataba wa kudumu. (Gazzetta dello Sport)

Barcelona wako tayari kuwauza beki wa Uruguay Ronald Araujo na winga wa Brazil Raphinha msimu huu wa joto ili kumleta mshambuliaji wa Athletic Bilbao na Uhispania Nico Williams, 21, Camp Nou. (SportsMole)

Chelsea wanamtaka mlinzi wa Nottingham Forest Murillo lakini wahahisi bei ya Mbrazili huyo ya pauni milioni 60 ipo juu sana. (Soka London)

Beki wa AC Milan Theo Hernandez anatarajiwa kukamilisha uhamisho wa £51m kwenda Manchester City. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 kwa sasa anaiwakilisha Ufaransa katika michuano ya Euro 2024. (Manchester Evening News)

Kiungo wa Chelsea Conor Gallagher "atasita" kuhamia Midlands ili kujiunga na Aston Villa huku Mwingereza huyo mwenye umri wa miaka 24 akisubiri mkataba mpya wa Blues. (Telegraph - usajili unahitajika)


Post a Comment

0 Comments