BETI NASI UTAJIRIKE

HISPANIA YATINGA ROBO FAINALI KIBABE

 Timu ya taifa ya Hispania imeendeleza ubabe baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Georgia mchezo wa hatua ya 16 bora michuano ya Euro 2024 . Kwa matokeo hayo Hispania imefanikiwa kutinga hatua ya robo fainali na itavaana na mwenyeji wa mashindano hayo Ujerumani tarehe 5 Julai.


katika mchezo huo Georgia walikuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza baada ya mchezaji wa Hispania Le Normand kujifunga dakika ya 18. Kiungo Rodri ndiye aliyesawazisha bao hilo dakika ya 39 na kuzifanya timu hizo kwenda mapumziko zikiwa zimefungana 1-1.

Felippe Ruiz aliipa Hispania bao la pili baada ya kupokea pasi kutoka kwa Lamine Yamal,Wiliam alifunga bao la 3 dakika ya 75 huku Olmo akihitimisha ushindi wa mabao 4 kwa kumalizia pasi iliyotoka kwa Oyarzabal dakika ya 83.

Hispania imecheza michezo mitatu katika hatua ya makundi ya michuano hiyo na kuvuna alama 9  kwa kupata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Crotia, ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Italy ,ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Albania na hatua ya mtoano imeshinda 4-1 dhidi ya Georgia.

Kiufundi timu ya hispania inamwenendo mzuri kwa kushinda mechi zote 4 na kufunga mabao 9 huku ikifungwa bao 1 tu.Ushindi huu wa Hispania unaifanya timu hiyo kuungana na Uswizi,Ujerumani,Uingereza katika hatua za robo fainali.

Post a Comment

0 Comments