ads

adds

TETESI ZA SOKA DUNIANI LEO TAREHE 15/01/2024

 Ajax wanaamini wanakaribia kukamilisha mkataba wa mkopo kwa kiungo wa kati wa Uingereza Jordan Henderson, 33, kutoka Al-Ettifaq ya Saudia. (Mirror)

Lakini Juventus pia wanavutiwa na Henderson na wana matumaini ya kumsaini nahodha huyo wa zamani wa Liverpool kwa mkataba wa awali wa miezi sita na chaguo la kufanya uhamisho huo kuwa wa kudumu. (Gazzetto dello Sport - kwa Kiitaliano)

Manchester United wanatumai kuanzisha mazungumzo na Benfica kuhusu mkataba wa majira ya joto kwa kiungo wa kati wa Ureno Joao Neves, 19, wiki chache zijazo (Mirror)

Sevilla bado wana matumaini ya kumsajili kiungo wa kati wa Tunisia Hannibal Mejbri kwa mkopo, ingawa Manchester United wangependelea mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 ajiunge na Everton . (Revolo - kwa Kihispania)

Fulham wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Porto kuwania saini ya mlinzi wa Uturuki wa Atletico Madrid mwenye umri wa miaka 27 Caglar Soyuncu. (A Bola via Sport Witness)

TH

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Juventus wameungana na Napoli na Galatasaray katika juhudi za kumsajili kiungo wa kati wa Nottingham Forest wa Ubelgiji Orel Mangala kwa mkopo. (Sky Germany)

Crystal Palace wanatumai kukamilisha dili la pauni milioni 10 kwa beki wa kulia wa Genk Daniel Munoz wa Colombia, 27. (Sun)

Sevilla wamekubali mkataba wa kumsaini mshambuliaji wa Manchester United mwenye umri wa miaka 20 kutoka Colombia Mateo Mejia kwa mkataba wa kudumu. (Fabrizio Romano)

Besiktas wamekataa ofa kutoka kwa Wolves kwa ajili ya mshambuliaji wao wa chini ya miaka 19 wa Uturuki Semih Kılıcsoy. (Haberturk - kwa Kituruki)

TH

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Jesse Lingard amemfuta kazi wakala wake huku mshambuliaji huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 31 akiendelea kutafuta klabu mpya baada ya kuachiliwa na Nottingham Forest. (Sky Sports)

Chelsea wako tayari kutumia kipengele cha ununuzi cha euro 60m (£52m) ili kumsajili winga wa umri wa miaka 16 wa Brazil wa chini ya umri wa miaka 17 Estevao Willian. (Sport - kwa Kihispania)

Fulham na Burnley wanavutiwa na beki wa kati wa Strasbourg Mfaransa Gerzino Nyamsi, 26. (Football Insider)

Kipa wa Manchester City wa Uingereza Ellie Roebuck, 24, yuko kwenye mazungumzo ya kina na mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa ya Wanawake Barcelona kuhusu uhamisho wa bure mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu huu. (Telegraph - usajili unahitajika)

Post a Comment

0 Comments