Vita mpya imeshaanza kwa msimu huu kati ya Kylian Mbappe anayekipiga PSG na Erling Halland anayekipiga Manchester City. kwa msimu wa 2021/22 Halaand na Mbappe waliweka rekodi nyingi kwa ligi zao za Ligue 1 Ufaransa na Bundesliga Ujerumani.
Rekodi ndani ya ligue 1 na EPL
Mpaka sasa nyota hawa wawili wameshaweka rekodi mpya kwa ligi wanazocheza .Mbappe akiwa na PSG ndiye mchezaji anayeongoza kwa mabao 7 akicheza mechi 6 sawa na mchezaji mwenza Neymar JR.Mabao hayo yameisaidia PSG kufikisha pointi 16 katika mechi 6 walizocheza.
Halaand ameanza vyema kwa msimu huu akifunga mabao 10 katika mechi 6 alizocheza huku akifunga Hat Trick mbili mfululizo. Mabao hayo yameisaidia timu ya Manchester City kufikisha pointi 14.
Rekodi michuano ya UEFA
Kwa msimu wa 2021/22 Kylian Mbappe akiwa na PSG aliweza kufunga mabao 6 kwenye michuno hiyo. Kwa msimu wa 2022/23 Mbappe ameshafunga mabao 2 dhidi ya Juventus . Matokeo hayo yanaifanya PSG kuongoza kundi H wakishinda mabao 2-1.Swali ni je Mbappe atamfunika Halaand kwa msimu huu?
Msimu wa 2021/22 Halaand akiwa na Borrusia Dortmund hakuwa na msimu mzuri. Kwa msimu wa 2022/23 Halaand amefanikiwa kufunga mabao 2 dhidi ya Sevilla .Matokeo hayo yanaifanya Manchester City kukaa kileleni mwa kundi G wakishinda mabao 4-0. swali ni Halaand atamfunika Mbappe.
Kwa msimu huu tusahau ile vita ya ronaldo na Messi na tuhamie kwenye hii vita nyingine itakayodumu kwa miaka 15 ijayo.
0 Comments