advertise with us

ADVERTISE HERE

HIZI HAPA SAJILI ZILIZOTIKISA VICHWA VYA HABARI ULAYA

 Pierre-Emerick Aubameyang

Chelsea imemsajili mshambuliaji Pierre-Emerick Aubameyang kwa mkataba wa £10.3m kutoka Barcelona na kiungo wa Juventus Denis Zakaria kwa mkopo.

Mshambulizi wa Gabon Aubameyang, 33, alifunga mabao 13 katika mechi 24 akiwa na Barca baada ya kujiunga na klabu hiyo ya Uhispania mwezi Februari akitokea Arsenal.



 

Wesley Fofana

th

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Msimu huu The Blues pia wameleta wachezaji tisa akiwemo beki wa Leicester Mfaransa Wesley Fofana kwa ada ya £70m, mshambuliaji wa Uingereza Raheem Sterling kutoka Manchester City kwa £50m, beki wa Senegal Kalidou Koulibaly kutoka Napoli kwa £34m, kiungo wa Uingereza Carney. Chukwuemeka kutoka Aston Villa kwa £20m, beki wa kushoto wa Uhispania Marc Cucurella kutoka Brighton kwa £62m.

th

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Idrissa Gueye, Manuel Akanii, Arthur Melo na Antony wahama siku ya mwisho

Everton ilisajili wachezaji kadhaa wa kati, huku mchezaji wa kimataifa wa Senegal Idrissa Gueye  akijiunga tena na The Toffees kutoka Paris St-Germain na James Garner akihama kutoka Manchester United.

Liverpool pia iliongeza kiungo kwenye kikosi huku mchezaji wa kimataifa wa Brazil Arthur Melo  akijiunga kwa mkopo wa msimu mzima kutoka Juventus. Leicester ilimsajili beki wa kati wa Ubelgiji Wout Faes kutoka klabu ya Ufaransa ya Reims kwa mkataba wa miaka mitano kuchukua nafasi ya Wesley Fofana, aliyejiunga na Chelsea kwa takriban £70m Jumatano.

Nottingham Forest ilisajili wachezaji watatu kutengeneza nyuso mpya 21 msimu huu wa joto, huku beki Loic Bade akiwa wa mwisho kuwasili kwa mkopo kutoka Rennes.

Marcos Alonso

th

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Beki wa kushoto Marcos Alonso ameondoka Chelsea kwa makubaliano na anatarajiwa kusaini na Barcelona.

Chelsea wana chaguo la kumsajili Zakaria kwa mkataba wa kudumu.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uswizi mwenye umri wa miaka 25 alijiunga na Juve tu kutoka Borussia Monchengladbach mwezi Januari.

Willian

th

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Fulham wamekamilisha usajili wa Willian kwa uhamisho wa bure, Carlos Vinicius kwa mkataba wa kudumu, pamoja na Dan James na Layvin Kurzawa kwa mkopo wa muda mrefu wa msimu.

Waliowasili wanaongeza idadi ya manunuzi yaliyofanywa na klabu hiyo ya Ligi Kuu msimu huu hadi 11.

Usajili wao wa mwisho kwenye dirisha hilo ulikuwa wa nyota wa  Wales James kutoka Leeds.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24

  Antony

th

Manchester United imemsajili winga wa Brazil Antony kutoka Ajax kwa ada ya awali ya euro 95m (£82m).

Mkataba huo, unaojumuisha uwezekano wa euro 5m (£4.3m) za nyongeza, ni usajili wa nne ghali zaidi katika historia ya Premier League.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 amesaini mkataba hadi 2027, na chaguo la mwaka wa ziada.

Hector Bellerin

th

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Beki wa Uhispania Hector Bellerin amekubali kurejea Barcelona kwa uhamisho wa bure  kutoka Arsenal.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27, ambaye aliichezea The Gunners michezo 239, atapewa kandarasi katika klabu yake ya utotoni hadi Juni 2023.

Beki wa pembeni wa Barca, Sergino Dest, anayedaiwa kuwindwa na Manchester United, amejiunga na AC Milan ya Italia kwa mkopo kwa muda wote uliosalia.

Post a Comment

0 Comments