BETI NASI UTAJIRIKE

AZAM WAKO TAYARI KUWABURUZA YANGA TAREHE 6

 Klabu ya Azam FC imeendelea na mazoezi makali mchana wa leo kujiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya bingwa mtetezi Yanga. Mchezo huo utapigwa jumanne ya tarehe 6 dimba la mkapa majira ya saa 1;00 usiku unategemewa kutoa taswira halisi ya vilabu hivyo kuelekea michuano ya kimataifa.


Mpaka sasa Azam FC wamecheza michezo miwili ya ligi kuu wakishinda mchezo dhidi ya kagera sugar kwa mabao 2-1 mabao yakiwekwa kimiani na Tepsi Evance na Prince Dube na ule wa sare ya 1-1 dhidi ya Geita Gold bao likifungwa na Tepsie Evance na wanapointi 4 huku Yanga wakishinda michezo yote miwili dhidi ya Polisi Tanzania uliomalizika kwa mabao 2-1 na mchezo wa pili dhidi ya Coastal Union uliomalizika kwa mabao 2-1.



Azam wameendelea na mazoezi makali uwanja wa azam complex na ndani ya mwezi huu watakuwa na michezo mitatu ya ligi kuu ikiwemo Mbeya City, yanga


Post a Comment

0 Comments