ads

adds

BWALYA ALIVYOONDOKA NA REKODI YA KIPEKEE SIMBA

 Kiungo Maestro Larry Bwalya ameagwa rasmi na klabu ya Simba na sasa ni mchezaji rasmi wa klabu ya Amazulu ya nchini Afrika Kusini. Nyota huyo alijiunga na wekundu wa msimbazi mwaka 2020 na ameitumikia klabu hiyo kwa mafanikio makubwa 


Bwalya alianzia soka lake katika klabu ya Zanaco FC ya nchini Zambia kwa msimu wa 2015-17 na baadaye alijiunga na Power Dynamos ya nchini humo msimu wa 2017-2020 na baadaye kujiunga na miamba ya Tanzania klabu ya Simba .

Akiwa ndani ya Simba ameisaidia klabu hiyo kutwaa kombe  ligi kuu,kombe la  FA,Kombe la Mapinduzi 1,Ngao za jamii mbili na alikuwa nyota tegemezi kwenye kikosi cha simba hasa msimu wa 2021/22 baada ya klabu hiyo kuwauza nyota wake Luis Miquissoine na Clatous Chota Chama.

Rally Bwalya baada ya mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo dhidi ya KMC Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam. ameaga vizuri akiisaidia timu kushinda 3-1

Post a Comment

0 Comments