ads

adds

KAMA WEWE NI MWANANCHI HILI LINAKUHUSU

 Kama wewe ni shabiki ,Mwanachama na Mpenzi wa Yanga una ujumbe wako maalumu hapa .Uongozi wa Yanga uliitisha kikao na wenyeviti wa matawi mbalimbali na kutoa mwongozo wa klabu hiyo 


kuelekea mfumo mpya wa kiuendeshaji.Moja ya ajenda kubwa kwenye mkutano huo ilikuwa ni kujadili ni namna gani klabu hiyo itajiongezea mapato na kuwa na mshikamano mzuri baina ya viongozi na mashabiki. Kikao hicho kilimalizika kwa makubaliano ya kwamba mashabiki wote wa Yanga ni lazima wawe na kadi za uanachama pamoja na kuwa na rasimu ya katiba ya mabadiliko.

Leo hii uongozi umetoa orodha ya matawi ya washiriki wote kwenye mkutano huo hivyo ni vyema kila mwanayanga ajitizame wapi anatoka na atawezaje kupata huduma za usajili pamoja na rasimu mpya ya mabadiliko ya kiuongozi.







Post a Comment

0 Comments