SIMBA YAVUNJA REKODI MAPOKEZI SONGEA

 


Klabu ya soka Simba imewasili mjini Songea kwa ajili ya mchezo wa nusu fainali kombe la Shirikisho la Azam (Azam Sports Federation) dhidi ya klabu ya Azam FC mchezo utakaopigwa uwanja wa majimaji. 

Simba iliondoka jijini Dar es salaam na shirika la ndege la Air Tanzania na ilipokelewa kwa kishindo ilipowasili mjini hapo kwa ajili ya mchezo huo wa tarehe 26 Juni majira ya saa 9:30 alasiri. Mshindi wa mchezo huo atacheza fainali ya michuano hiyo kwa msimu wa 2020/21.

Hizi ni baadhi ya picha za timu hiyo ilipowasili mjini Songea na  kulakiwa na mashabiki lukuki 







Post a Comment

0 Comments