TETESI ZA SOKA DUNIANI LEO TAREHE 18-12-2020

Juventus wameanza kufanya mazungumzo na wakala wa Paul Pogba, 27, Mino Raiola wakijiandaa kumsajili tena kiungo huyo wa kati wa Manchester. (Express)

Mlinzi wa Chelsea na England Fikayo Tomori, 22, ambaye amehusishwa na Leeds, anajiandaa kujiunga na klabu ya Ufaransa ya Rennes kwa mkopo hadi mwesho wa msimu. (Talksport)

Liverpool wanamnya kiungo wa kati wa Lille na Portugal Renato Sanches, 23. (Le10 Sport - in French)

Liverpool wanamyatia kiungo wa kati wa Lille na Portugal Renato Sanches(Kulia)

Huenda wakamnunua Sanches kujaza pengo lililoachwa Georginio Wijnaldum, ambaye Liverpool hawana nia ya kumuachilia, japo hawako hawajaridhia ombi la kiungo huyo wa kati wa Uholanzi aliye na umri wa miaka 30, la kutaka mkataba wa miaka minne. (Express)

Manchester United watasubiri hadi Januar kuamua ikiwa watamuachilia mchezaji wao wa safu ya kushoto na nyuma Brandon Williams ,20, - ambaye ananyatiwa na Southampton na Newcastle - kuondoka kwa mkopo. (Manchester Evening News)Chelsea wana imani watasalia na Olivier Giroud mwezi Januari na kuendelea kumhakikishia mshambuliaji huyo aliye na umri wa miaka 34- kwamba atasalia na nafasi yake katika kikosi cha kitaifa cha Ufaransa katika michuano ya Ulaya . (Telegraph - subscription required

Olivier Giroud

Manchester United bado wanamtafuta winga mahiri na wachezaji wa safu ya kati na nyuma na vile vile safu ya ulinzi japo matumaini yako lakini hhawatawasajili wachezaji wapya mwezi Januari dirisha la uhamisho litakapofunguliwa. (Manchester Evening News)

Mshambuliaji wa Paris St-Germain Neymar amepuuzilia mbali tetesi kuwa huenda akarejea Barcelona, huku nyota huyo wa Brazil aliye na umri wa miaka 28- akisisitiza kuwa ameridhika kuwa mjini Paris. (Express)

Angel di Maria and Neymar
Maelezo ya picha,

Manchester United wamefufua matumaini ya kumsaka kiungo wa kati wa Atletico Madrid na Uispania Saul Niguez, 26. (Todo Fichajes, via Team Talk)

Arsenal huenda wakamnunua kiungo wakati wa Porto Mreno Fabio Vieira mweiz Januari na wako tayari kulipa ada £27m ili kumwezesha kuvunja mkataba wake wa sasa. (Record, via Mail)

Mkufunzi wa Arsenal Mikel Arteta amewaomba maafisa wa klabu hiyo kuwasajili kiungo wa kati wa Real Madrid na Uhispania Isco, 28, na kiungo wa kati wa Lyon na Ufaransa Houssem Aouar, 22, mwezi Januari. (Defensa Central, via Team Talk)

Manchester United wamefufua matumaini ya kumsaka kiungo wa kati wa Atletico Madrid na Uispania Saul Niguez
Maelezo ya picha,


Post a Comment

0 Comments