advertise with us

ADVERTISE HERE

WOLVES, BAYERN NA SEVILLA ZAIFUATA MANCHESTER UNITED


Klabu za Sevilla ,Bayern leverkusen ,Sevilla na Basel zimeungana na Manchester United,Intermilan,Copenhagen na Shakhtar Doneski hatua ya robo fainali kwenye mchuano ya Europa League. 

Wolves waliibuka na ushindi wa jumla ya mabao 2-1 baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 kwenye mchezo uliochezwa hapo jana na kuifanya timu hiyo kucheza na Sevilla mchezo wa robo fainali.

Leverkusen wao watavaana na Intermilan baada ya kuibuka bao 1-0 dhidi ya rangers huku wakiwa na uwiano wa ushindi wa mabao 4-1. Kwa upande mwingine klabu ya Manchester United itavaana na Copenhagen huku Sharkter wakivaana na Basel . 

Michezo hiyo itapiigwa kwa raundi moja tu na timu zote zitacheza michezo yao kwenye viwanja mbalimbali nchini ujerumani.Michezo hiyo itapigwa tarehe 10 na 11 mwezi Agosti

Post a Comment

0 Comments