advertise with us

ADVERTISE HERE

TETESI ZA SOKA DUNIANI LEO JUMANNE TAREHE 11-08-2020


Aaron Ramsey hajamridhisha kocha Andrea Pirlo wa Juventus. Kingo huyo wa kati wa kimataifa wa Wales mwenye umri wa miaka 29 yuko huru kuhamia klabu nyingine. (Mirror)
Inter Milan wanamlenga beki wa Manchester United Chris Smalling, 30, wakati wa uhamisho. (Gazzetta dello Sport)
Manchester United wanaendelea na juhudi za kumsaka winga wa kimataifa wa England Jadon Sancho licha ya Borussia Dortmund kusisitiza kuwa nyota huyo wa miaka 20- atasalia katika klabu hiyo msimu ujao. (Mail)
Jadon Sancho
Maelezo ya picha,
Kiungo wa kati wa JuventusBlaise Matuidi, 33, atajiunga na Inter Miami inayoshiriki ligi ya MLS akisubiri akisubiri matokeo ya uchunguzi wa kimatibabu . (Goal)
Arsenal wanakaribia kukamilisha mchakato wa kumsajili kiungo wa zamani wa Chelsea Willian,32, baada ya nyota huyo wa Brazil kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu. (Standard)
Chelsea wamekubali kumpatia mkataba wa miaka mitano mshambuliaji wa Bayer Leverkusen na Ujerumani Kai Havertz lakini wamefahamishwa kuwa kiungo huyo wa miaka 21- atawagharimu £90m. (RMC Sport - via Sun)
Kai Havertz
Maelezo ya picha,
Chelsea wanakakabiliwa na ushindani mkali kutoka kwa Lazio katika kinyang'anyoro cha kumsaini beki wa Real Madrid Mhispania Sergio Reguilon, 23. (DiMarzio)
Manchester City watapokea ada ya £8m kumuachilia mlinzi wa kati wa Argentina Nicolas Otamendi,32, msimu huu wa joto. (Sun)
Newcastle wanajiandaa kumenyana na AC Milan na Roma kumsajili kiungo wakati wa Burnley Jeff Hendrick, 28. (Guardian - via Mail)
Nicolas Otamendi
Maelezo ya picha,
Wolves wana imani mkufunzi wao Nuno Espirito Santo atasaini mkataba mpya kabla ya msimu mpya wa ligi kuu ya primia. (90Min)
Leicester City wanamfuatilia winga wa Barcelona na Portugal Francisco Trincao, 20. (Fabrizio Romano - via Leicester Mercury)
Aston Villa na Crystal Palace wamehusishwa na uhamisho wa kiungo mahiri wa Norwich Muargentina Emiliano Buendía, 23. (HITC via Sun)

Post a Comment

0 Comments