ads

adds

SWALA LA NGASA NI PASUA KICHWA KWA MASHABIKI NA VIONGOZI WA YANGA


Mashabiki mbalimbali wa soka nchini hususani mashabiki wa Yanga wameutaka uongozi wa klabu hiyo kufanya maamuzi mapya ya kumrudisha mkongwe wake Mrisho Ngassa. Klabu hiyo ilitangaza kuachana na nyota wake 14 huku ngasa akiwa mmoja wao.

Kupitia mitandao ya kijamii mashabiki mbalimbali wameunga mkono kampeni mpya iitwayo BRING BACK NGASSA yenye nia ya kurudisha mchezaji huyo mkongwe klabuni hapo. Ngassa amekuwa na Yanga kwenye nyakati ngumu na za kufurahisha 

Ngassa aliitumikia Yanga kipindi cha neema ikiwa chini ya mwenyekiti wao Yusuf Manji na sasa ameitumikia timu hiyo kwenye nyakati ngumu  za mwenyekiti Mshindo msolla.Mahabiki wa klabu hiyo wanaamini ngassa ni mchezaji mkongwe n anajua nii anafanya akiwa ndani ya uwanja 

Swali linabaki je  Ngassa arudishwe Yanga au aachane nao? 

Post a Comment

0 Comments