Klabu ya Simba SC imetangaza kwamba klabu ya VitalO ya Burundi ndiyo mgeni mwalikwa wa Simba day na ndiyo klabu itakayocheza mchezo wa kirafiki siku ya Jumamos Agosti 22 mchezo utakaopigwa dimba la Benjamini mkapa jijini Dar es Salaam. Klabu ya Simba husherehekea Simba Day kila tarehe 8 August lakini kwa mwaka huu zoezi lilishindikana kutokana na mabadiliko ya ratiba ya ligi kuu kuchelewa kumalizika kutokana na janga la corona. Simba wamefanikiwa kutwaa mataji matatu kwa msimu wa 2019/20 na sherehe hizo zinategemewa kupambwa na makombe hayo huku pia mechi hiyo ikitumika kuwatambulisha nyota kadhaa waliosajiliwa msimu huu akiwemo wakili msomi Benard Morrison ,Ibrahim Ame ,Onyango,Bwalya na wengine .
Post a Comment
0
Comments
MERIDIAN BET
EURO 2024
Kuanzia tarehe 14 june to 14 july AMOSPOTIXTRA TEAM itakuwa ujerumani kukuletea michuano ya EURO2024
0 Comments