ads

adds

NAMUNGO WAZUNGUMZIA WALIVYOJIPANGA KWA MSIMU WA 2020/21



Mwenyekiti wa Namungo FC Hassan Zidadu, alisema kuwa wameshaanza mchakato wa kusajili wachezaji wapya ili kukiongezea nguvu kikosi hicho.Namungo ilimaliza ligi kuu Tanzania Bara ikiwa nafasi a nne huku ikiingia fainali ya FA mchezo waliopoteza kwa mabao 2-1 dhidi ya Simba. Zidadu amenukuliwa akisema

Tupo kwenye mpango wa kusajili wachezaji wapya na kila kitu kinaenda sawa kwa kuanza na kuwaongezea mkataba wale ambao muda wao umeisha pamoja na kuongeza wengine nane kwa mujibu wa ripoti ya Kocha Mkuu.

“Tutaiwakilisha nchi kimataifa, hivyo lazima usajili wetu uwe wa kimataifa zaidi ili tuweze kupeperusha Bendera ya Taifa, mashabiki wasihofie, tupo kamili,” 

Post a Comment

0 Comments