MCHEZAJI MPYA WA BARCELONA AKUTWA NA CORONA


Mchezaji mpya wa Barcelona Miralem Pjanic amekutwa na virusi vya Corona. Pjanic alihama kutoka Juventus kama dili la mabadilishano na mchezaji raia wa brazil Arthur mwezi juni na ataanza kucheza rasmi msimu wa 2019/20. 

Mchezaji huyo mwenye miaka 30 atajiunga na mazoezi ya timu hiyo baada ya siku 15 baada ya kujitenga na wachezaji wenzake wa Barcelona.Klabu hiyo ilichapisha picha  ya mchezaji huyo ikimpa pole na kumtakia arejee uwanjani mapema.

Pjanic ameondoka Juventus akiwa na makombe manne ya Serie A kombe la Italia mara mbili.

Post a Comment

0 Comments