Kocha mkuu wa Arsenal ameweka rekodi mpya kwenye michuano ya FA nchini uingereza baada ya kuibuka kidedea kwenye fainali ngumu iliyopigwa dimba la Wembley jijini London. Kwenye mchezo huo mzuri wa kuvutia Arsenal waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 na shukrani za pekee zimwendee Piere Aubemayang aliyefunga mabao yote mawili. Mikel Arteta anakuwa kocha wa kwanza kutwaa kombe la FA akiwa mchezaji wa klabu ya Arsenal na akiwa kocha wa klabu hiyo. Hakuna kocha yeyote aliyewahi kuweka rekodi kama hiyo mpaka sasa. Itakumbukwa kocha huyo alikabidhiwa timu hiyo Disemba 2019 baada ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo Unai Emery kushindwa kuiongoza kufanya vizuri kwa timu hiyo kwa misimu miwili mfululizo.
Post a Comment
0
Comments
MERIDIAN BET
EURO 2024
Kuanzia tarehe 14 june to 14 july AMOSPOTIXTRA TEAM itakuwa ujerumani kukuletea michuano ya EURO2024
0 Comments