advertise with us

ADVERTISE HERE

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE TAREHE 14-07-2020


Rais wa Barcelona Josep Maria Bartomeu amekataa uwezekano wa mshambuliaji wa Paris St-Germain Neymar,28, kurejea Nou Camp lakini amesema klabu inafikiria uhamisho wa mshambuliajji wa Inter Milan Muajentina Laitaro Martinez, 22. (TV3 Mundo Deportivo)
Bartomeu pia amesema ana ''uhakika'' mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi,33, atasalia Nou Camp zaidi ya mwaka ujao. (TV3 via Evening Standard)
Manchester City itatoa ofa kwa kocha Pep Guardiola ya mkataba wa muda muda mrefu baada ya marufuku dhidi ya klabu hiyo kufutwa. (Mirror)
Pep Guardiola
Guardiola atapatiwa karibu kitita cha pauni milioni 150 kwa ajili ya kukipa nguvu kikosi cha City. (Guradian)
Real Madrid inaamini kuwa mshambuliaji Kylian Mbappe ,21, atakuwa na mazungumzo nao kuhusu uhamisho kutoka Paris St-Germain. (Marca)
Liverpool ina mpango wa kumuuza beki wake Dejan Lovren,31, ingawa anatafuta kuongeza mkataba wake. (Goal)
Kylian Mbappe
Bayern Munich wanajiandaa kuanza mchakato wa kumnasa Tanguy Ndombele ,23, wa Tottenham na Mfaransa mwenzie anayecheza katika nafasi ya kiungo cha kati katika klabu ya Monaco, Tiemoue Bakayoko,25. (Le 10 Sport via Daily Mail)
Nice imetoa ofa kwa kiungo wa kati Mhispania Rony Lopes anayekipiga Sevilla. (RMC Sport-in French)
Mkurugenzi wa michezo katika klabu ya Norwich Stuart Webber amesema kwamba kandarasi ombi la kutaka kumnunua mchezaji kinda mwenye kipaji mwisho wa msimu litaanza kwa dau la £20m . (Norwich Evening News)
Mourinho na Tanguy Ndombele
Brentford inamlenga winga wa Portsmouth Ronan Curtis,24 kwa ajili ya kuchukua nafasi ya Said Benrahma ikiwa ataondoka kwenye klabu hiyo. (The News, Portsmouth)

Post a Comment

0 Comments