ads

adds

TETESI ZA SOKA DUNIANI LEO JUMANNE TAREHE 14-07-2020


Inter Milan wanafikiria kumnunua kiungo wa kati, Mfaransa N'Golo Kante huku Blues wakiwa tayari kusikiliza ofa kwa ajili ya kumuuza mchezaji huyo wa Ufaransa, 29. (Gazzetta dello Sport, via Metro)
Zenit St Petersburg wameeleza nia yao ya kumsajili beki anayekipiga katika klabu ya Liverpool Dejan Lovren, 31. (Liverpool Echo)
AC Milan wanafiukiria kumnunua mashambuliaji wa Real Madrid raia wa Serbia Luca Jovic, 22, ambaye anatekodolewa macho na Leicester City na Arsenal. (Calciomercato,via Leicester Mercury)
Luca Jovic
Kai Havertz anataka kuondoka Bayer Leverkusen kwasababu walishindwa kufuzu katika michunao ya klabu bingwa Ulaya hivyobasi Chelsea watalazimika kuhakikisha wanafuzu katika michuano hiyo ili kumshawishi kiungo huyo wa Ujerumain 21 kujiunga na timu hiyo.. (Bild)
Bayern Munich wana mpango wa kuwanasa viungo wawili wanaocheza ligi kuu ya Ufaransa, Tonguy Ndombele wa Tottenham, 23, na Tiemoue Bakayoko. (Le 10Sport)
Mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic, 38, amesema hana uhakika kuhusu mustakabali wake ndani ya AC Milan kwa kuwa hakuna mazungumzo yoyote yaliofanyika kuhusu mkataba ikiwa sasa ni chini ya mwezi mmoja kabla ya mkataba wake kufikia ukingoni. (Sky Sports)
Tonguy Ndombele
Mashabiki 5,000 waliruhusiwa kuingia uwanjani kutazama mechi ya kirafiki ya Paris St Germain, mechi iliyoitoa kifua mbele kwa 9-0 dhidi ya wenyeji Le Havre. (France 24)

Post a Comment

0 Comments