advertise with us

ADVERTISE HERE

REAL MADRID WAENDELEA KUTIKISA LA LIGA


Klabu ya Real madrid imeendelea kusailia kileleni mwa msimamo wa La Liga kwa tofauti ya pointi 4 dhidi ya Barcelona baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Alaves. Karim Benzema alikuwa wa kwanza kuipa Real Madrid bao la kuongoza baada ya kufunga kwa mkwaju wa penati dakika ya 11 huku Asensio akikamiliha ushindi kwa bao la pili dakika ya 51.

Matokeo hayo yanawafanya Real Madrid kufikisha pointi 80 wakicheza michezo 35 huku wakitakiwa kupata ushindi kwenye michezo ya Granada na Villareal ili kuweza kutawagazwa mabingwa wapya wa La Liga msimu wa 2019/20

Post a Comment

0 Comments