advertise with us

ADVERTISE HERE

MANCHESTER UNITED YAWASAMBARATISHA AKINA SAMATTA YAWEKA REKODI MPYA


Klabu ya Manchester United imeendelea kuweka rekodi mpya ligi kuu nchini Uingereza baada ya kushinda mchezo dhidi ya Aston villa.Manchester United waliibuka na ushindi wa mabao 3-0 yaliyofungwa na B.Fernandez dakika ya 27 kwa mkwaju wa penati ,Mason Greenwood dakika ya 45 ya mchezo huo na kuwafanya Manchester United kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-0.

Kiungo Paul Pogba aliipa manchester United bao la 3 dakika ya 58 na kuifanya klabu hiyo ifikishe pointi 58 nyuma ya Leicester City waliopo nafasi ya 4 wakiwa na pointi 59. 

Rekodi mpya 

Kitendo cha Manchester kushinda mechi 4 mfululizo tena kuanzia mabao matatu kunaifanya klabu hiyo kuweka rekodi kuwa klabu ya kwanza kushinda mechi nne mfululizo kwa idadi kubwa ya mabao.

Manchester United ilishida 3-0 dhidi ya Shiffield ,3-0 dhidi ya 3-0 dhidi ya Brighton ,5-2 dhidi ya Bournemouth na 3-0 dhidi ya Aston Villa 

Post a Comment

0 Comments