advertise with us

ADVERTISE HERE

JUVENTUS YAPIGWA COMEBACK YA HATARI HUKU ZLATAN NA RONALDO WAKIFUNGA


Wachezaji wa Juventus wamejikuta wakipigwa butwaa baaa ya kufungwa mabao 4-2 na Ac Millan mechi iliyopigwa dimba la San Siro jijini Milan. Juventus walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia Adrien Rabbiot dakika ya 47 kipindi cha pili huku Ronaldo akifunga bao la pili dakika ya 53.

Ac Milan walipata penati dakika ya 62 na Ibrahimovich alifunga penati hiyo huku Frenc Kessie akisawazisha dakika ya 66 Rafael Reao akapiga bao la tatu  dakika ya 67 na Ante Rebic akifunga bao la 4 dakika ya 80. Mpaka mpira unamalizika matokeo yalikuwa ni AC Milan 4 na Juventus 2

Matokeo hayo yanaifanya Ac Milan kupanda mpaka nafasi ya 5 ikifikisha pointi 49 huku Juventus akisalia nafasi ya 1 akiwa na pointi 75. Hii inakuwa ni comeback bora zaidi tangu kurejea kwa serie A msimu huu 

Post a Comment

0 Comments